IQNA

Mkutano wa Umoja wa Kiislamu wafanyika Guinea Conakry

0:07 - December 03, 2016
Habari ID: 3470711
IQNA-Mkutano wa kitaifa wa Umoja wa Kiislamu umefanyika kwa mara ya kwanza nchini Guinea Conakry.
Kwa mujibu wa mwandishi wa IQNA, mkutano huo umefanyika katika ukumbi mkubwa wa mikutano katika mji mkuu wa Guinea Conakry kwa kushiriki Jumuiya ya Kimataifa ya Kukurubisha Madhehebu za Kiislamu na himaya Ubalozi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran nchini humo.
Katika mkutano huo, zaidi wa maulamaa, wahubiri, maimamu na mashekhe 1500 wa Ahul Sunna wal Jamaa, Mashia, na viongozi wa Tariqa ya Tijaniyya kutoka kote Guinea Conakry walishiriki katika mkutano huo.
Kongamano hilo lilidhuhduriwa na Abdulkarim Chubati ambaye ameitaja Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kuwa nchi yenye kueneza Umoja wa Kiislamu.
Aidha kikao hicho kilihutubiwa na Hujjatul Islam wal Muslimin Dkt. Sayyid Mahmoud Waziri,  mwakilishi wa  Ayatullah Makarim Shirazi na Ayatullah Safi Golpaygani, marajii wa Waislamu wa madhehebu ya Shia.
Dkt. Waziri ameashiria aya za Qur'ani Tukufu kuhusu umoja na kusema moja ya nukta muhimu hivi leo ni umoja baina ya Waislamu.
Aidha mkutano huo ulihutubiwa na  Hujjatul Islam wal Muslimin Wasti, mwakilishi wa Jumuiya ya Kimataifa ya Kukurubisha Madhehebu za Kiislamu yenye makao yake mjini Tehran.

3550314/
captcha