Rawdah Tukufu iko kati ya Chumba Kitukufu (kinachojulikana kama nyumba ya Mtume), na Minbar ya Mtume Muhammad (SAW). Sehemu hii ya kusini-mashariki ya Al-Masjid an-Nabawi ndipo nyumba ya mtukufu huyo iliposimama, ambapo aliishi na kuzikwa. Ni ya thamani kubwa sana ya kidini kwa Waislamu.
Kati ya waumini hao, 2,273,033 walikuwa wanawake na 1,149,364 walikuwa wanaume, vyombo vya habari vya Saudia viliripoti Jumatano.
Jumla ya waumini 4,125,257 waliofika hapo kwa ajili ya Hija ndogo ya Umrah pia walitoa heshima zao kwa Mtume Muhammad SAW na masahaba zake wawili Abu Bakr Al-Siddiq na Umar ibn Al-Khattab.
Halikadhalika milo 825,000 ya futari ilitolewa kwa wageni wa Al-Masjid an-Nabawi katika kipindi hicho na waumini milioni 1.2 walinufaika na huduma za tafsiri katika lugha kumi tofauti ambazo zilitolewa kupitia tovuti zilizo eneo hilo.
Mwaka wa sasa wa Hijri ulianza tarehe 30 Julai 2022.
3480079