Dua hizi za kila siku za Mwezi wa Ramadhani husomwa toka mwanzo ya tarehe mosi Ramadhani hadi siku ya mwisho katika mwezi huu mtukufu. Kila dua ina siku yake, na inaweza kusomwa mara nyingi kadiri ya uwezo wa mtu mwenyewe.
Ee Mwenyezi Mungu! Nijaalie katika mwezi huu niwe miongoni mwa wanaoomba maghfira (kwa wingi), pia nijaalie niwe miongoni mwa waja wako wema walio wanyenyekevu, Unijaalie niwe miongoni mwa watu wako walio karibu nawe kwa huruma yako Ewe Mhurumivu wa wanaohurumia.