IQNA

Awamu ya Mwisho ya Mashindano ya 25 ya Kitaifa ya Qur'ani ya Lebanon yakamilika

17:14 - November 30, 2022
Habari ID: 3476175
TEHRAN (IQNA) – Duru ya mwisho ya Mashindano ya 25 ya Kitaifa ya Qur’ani nchini Lebanon ilifanyika mjini Beirut Jumapili, Novemba 27.

Jumla ya washiriki 120 walishiriki katika toleo hili la hafla hiyo. Kategoria hizo ni pamoja na kisomo na kuhifadhi Qur'ani nzima, 10 Juzuu (sehemu), 15 Juzuu, na 20 Juzuu.

Washiriki wa kiume walishiriki katika usomaji wa Tahqiq wakati shindano la kusoma Tarteel ni la wanawake. Shindano hilo limeandaliwa na Jumuiya ya Tawjih na Irshad (miongozo na ushauri) ya Lebanon. Mchanganyiko wa mbinu ushiriki wa intaneti na za ana kwa ana zilitumika katika toleo hili la tukio. Hatua ya awali ilifanyika Novemba 10-13. Washindi watatangazwa hivi karibuni na jopo la waamuzi.

 

4103285

captcha